Hail, Caesar ni movie yenye comedy,drama na music ambayo imetayarishwa kwa ustadi mkubwa, ikielezea maisha ya watengeneza filamu na mikasa wanayokutana nayo wakati wa utengenezaji wa filamu hizo. Mkasa mkubwa katika filamu hii ni pale Muigizaji mkuu wa filamu iliyokuwa inaandaliwa kutekwa.
Hail, Caesar! itaoneshwa kwa mara ya kwanza tarehe 5/2/ 2016. Starrings: Josh Brolin, George Clooney, Scarlett Johansson, Channing Tatum, Ralph Fiennes, Jonah Hill, Frances McDormand, Tilda Swinton, Dolph Lundgren, na wengine wengi.
Kwa wapenzi wa games za X-BOX, angalia Trailer ya gemu ya Halo 5: Guardians itakayoanza kupatikana tarehe 27 mwezi huu kwa x-box one.
Game hii imeandliwa na kampuni ya Microsoft wakishirikina na 343 studios. Kama ni mpenzi wa games hizi unaweza weka pre-order HAPA
Moja ya Filamu kali zilizotoka mwaka huu zinazohusu teknolojia ni nyingi ila chache kati ya hizo ni Blackhat, Furious 7 na CHAPPiE.
CHAPPiE ni Filamu iliyoigizwa nchini Afrika Kusini,Ambapo inaelezwa kwamba baada ya nchi hiyo kuchoshwa na vitendo mbalimbali vya uharifu katika jiji la Johannesburg, serikali yake inachukua uamuzi wa kununua teknolojia ya roboti wenye uwezo mkubwa wa kufikiri (Artificial Intelligence ) ili kulisaidia jeshi la polisi kukabiliana na matatizo hayo.
Lakini hapo badae mgunduzi (Dev patel) wa roboti hizo anataka kujribu mfumo mpya (Program) ambao utawanya roboti hao kuwa na hisia na makuzi kama ya binadamu lakini Bosi wake anamkatalia kujaribu mfumo huo.
Ndipo anapoiba roboti moja lililoaribika ilikujaribu huo mfumo, na hapo ndipo matatizo yanapoanza.
Filamu hii imechezwa na waigizaji maarufu kama Dev Patel ( ameigiza katika filamu ya Slumdog Millionaire ya 2008), Hugh Michael Jackman (Ameigiza filamu za X-men) na wengine wengi.
Itafute movie hii uitazame, NI KALI SANA.
Kama wewe ni mfuatiliaji mzuri wa Filamu, hakika filamu ya Furious 7 itakuwa ni moja kati ya filamu ambazo hazichoshi kuangalia. Wengi wamekuwa wakijiuliza Jinsi Filamu hiyo ilivyo tengenezwa, Ukweli ni kwamba vipande vingi vya Filamu hiyo vilichukuliwa katika mazingira ya ukweli. Mfano ni kipande hiki ambacho Paul Walker’s Brian aliruka katika gari (Bus) liliokuwa linadondoka katika bonde kali. Tazama Video hii kuona jinsi Furious 7 ilivyotengenezwa.
Kumekuwa na vikwazo vingi vinavyosababisha wanafunzi kushindwa kufanya majaribio ya kutosha ya masomo wanayosoma.
Vikwazo hivyo ni pamoja na mda mdogo mashuleni, wazazi kushindwa kuyamudu masomo wanayosoma watoto wao na kadharika.
NIPIME ni programu tumishi inayowezesha wanafunzi wa sekondari kufanya majaribio ya hesabu na fizikia kwa kutumia simu zenye mfumo wa android. Mtumiaji wa nipime hufanya jaribio moja lenye maswali matano kisha majibu yake huhakikiwa kama ni ya sahihi au siyo.
Baadae, programu hiyo huonesha alama (maksi) alizopata mtumiaji huyo kulingana na maswali aliyojibu sahihi.
Mtumiaji haitaji kuwa na mtandao wa internet ili kutumia programu hii, jambo linaloifanya programu hii kuwa ya pekee kwa kujali uchumi wa wanafunzi na wazazi pia.
Pia programu hii inaonesha ni kwa kiasi gani teknolojia inaweza leta mabadiliko katika nyanja ya elimu Tanzania, kwani sasa mzazi yeyote bila kujali kiwango chake cha elimu anaweza mpa mwanae majaribio mbalimbali na kuyafanya.
Programu hii inapatikana Play store kwa jina la nipime, BOFYA HAPA kuipakua Au kupitia tovuti maalumu kwaajili ya programu hii: nipime.edumek.com
This song"NANA"Has Been Produced By Naahreal From Tanzania And Writen By Diamond Platnumz And Mr Flavour'The Video Was Shoot In Cape Town,South Africa By Godfather Production.