Showing posts with label Misri. Show all posts
Showing posts with label Misri. Show all posts

Monday, September 14, 2015

Misri yaomba radhi

No comments

Misri imeomba radhi baada ya watu 12, wakiwemo watalii raia wa Mexico kuuawa kwa bahati mbaya na vikosi vya usalama wakati wa Operesheni dhidi ya ugaidi.

Wizara ya mambo ya ndani ya Misri imedai kuwa kundi hilo la watu liliingia kwenye eneo lililopigwa marufuku.

Nchi hiyo imekuwa ikipambana na wanamgambo wa kiislamu kwa miaka kadhaa huku mashambulizi yakishika kasi tangu kuondolewa madarakani kwa Rais Mohammed Morsi mwaka 2013.

Mbali na kuwa jangwa la magharibi ni kivutio cha utalii, limekuwa la hatari kwasababu ya kuzorota kwa usalama nchini Libya.

Raia kumi wa Mexico na wa Misri walijeruhiwa katika operesheni hiyo.Maafisa usalama wamesema idadi ya watalii wa Mexico waliouawa ni wanane na wamisri wanne ingawa idadi hiyo ya Raia wa Mexico haijathibitishwa na Mexico yenyewe.

Waziri Mkuu wa Misri,Ibrahim Mahlab ameomba radhi kwa njia ya simu alipozungumza na Balozi wa Mexico jijini Cairo,Al-Yawm al-Sabi.Tovuti ya nchi hiyo ilimnukuu.

Chanzo:BBC Swahili  

read more

Friday, August 07, 2015

Muda wa mwisho uliotangazwa na wanajihadi wamalizika Misri

No comments

baada ya muda wa mwisho kupita.

Wizara ya mambo ya kigeni ya Misri imesema inafanya juhudi za hali ya juu kumtafuta Tomislav Salopek , mfanyakazi wa kampuni ya kigeni ya utafutaji wa mafuta mwenye umri wa miaka 31 aliyetekwa nyara mwezi uliopita.

Slopek ameonekana katika ukanda wa video wa kundi hilo la IS uliotolewa katika mtandao wa Internet siku ya Jumatano, akiwa amepiga magoti karibu na mtu aliyejifunika uso akiwa ameshika kisu.

Alisoma kikaratasi kwamba watekaji nyara wake watamuua katika muda wa saa 48 iwapo serikali ya Misri itashindwa kuwaachia huru wanawake walioko magerezani, sharti kuu la wanamgambo hao wa Kiislamu katika muda wa miaka miwili iliyopita.

Video hiyo haikufafanua ni wakati gani muda huo wa mwisho ulianzia, lakini zaidi ya masaa 48 yamepita tangu video hiyo kuwekwa mtandaoni, na hakuna taarifa mapema leo Jumamosi juu ya iwapo hatua ya kuuwawa mtu huyo imetekelezwa.

Raia wa kigeni wanahofu

Utekaji nyara huo ambao haukutarajiwa nchini Misri -- umewatisha raia wa kigeni wanaofanyakazi katika makampuni ya kimataifa na kuonesha uwezo wa makundi ya Jihadi , licha ya kampeni kubwa ya kijeshi dhidi ya kundi hilo la IS.

Licha ya kuwa imekuwa ikipambana na wapiganaji wa IS katika eneo hilo la rasi ya Sinai linaloishi watu wachache, taifa hilo la Afrika kaskazini limekuwa halijakumbana na kadhia ya utekaji nyara wa raia wa kigeni na mauaji ya kinyama yanayofanywa na wapiganaji wa jihadi nchini Syria na Libya.

Baba yake Salopek ametoa wito kwa wateka nyara kumwachia mwanae , baba wa watoto wawili, wakati waziri wa mambo ya kigeni wa Croatia Vesna Pusic amesafiri kwenda Cairo kwa mazungumzo ya dharura.

"Nawaomba watu ambao wanamshikilia mwanangu kumruhusu arejee katika familia yake, kwasababu nia yake kwenda katika nchi yenu ilikuwa tu ni kwa madhumuni ya kupata riziki yake na watoto wake.

Hakuna zaidi," Zlatko Salopek ameliambia shirika la habari la AFP nyumbani kwake katika mji wa mashariki nchini Croatia wa Vrpolje.

Waziri wa Croatia aenda Misri

Baada ya mazungumzo kati ya waziri wa mambo ya kigeni wa Misri Sameh Shoukry na Pusic , serikali ya Misri imesema: "Hatutasita kuchukua hatua yoyote kumtafuta na kumpata mateka huyo na uhakika wa usalama wake."

Maelfu ya watu , wengi wao wafuasi wa mrengo wa Kiislamu , wamefungwa jela tangu jeshi kumpindua kutoka madarakani rais mwenye msimamo wa itikadi ya dini ya Kiislamu Mohammed Mursi mwaka 2013 na kuanzisha ukandamizaji uliosababisha vifo kwa waungaji wake mkono.

Salopek alitekwa nyara mwezi uliopita katika barabara kutoka magharibi ya Cairo. Dereva wake ameachiwa bila kudhurika , na polisi imesema wamemhoji.

Katika mji anakotoka Salopek , majirani wanasubiri taarifa kuhusu Salopek , wakimweleza kuwa ni kijana mcheshi.

Chanzo: DW Swahili

read more